
Maandamano yalifanyuika baada ya ubakaji huo mjini Delhi kulaani kitndo hicho cha unyama
Mshukiwa katika kesi ya ubakaji
wa msichana mmoja wa chuo kikuu ambaye baadaye alifariki nchini India,
amepatikana amefariki gerezani. Haya yamethibitishwa na wakili wake.
Polisi wanasema kuwa Ram Singh, alijinyonga
akiwa ndani ya gereza la Tihar mjini Delhi's Tihar, lakini mawakili wa
utetezi wanadai kuwa huenda alinyongwa.Wote walikanusha madai hayo.
Shambulizi dhidi ya mwanafunzi huo, lililofanyika Disemba mwaka jana, lilizua mjadala mkali nchini India kuhusu wanawake wanavyodhulumiwa.

Jela la Tahir ambako washukiwa wa ubakaji wanazuiliwa
Mwandishi wa BBC Sanjoy Majumder,mjini Delhi,anasema kuwa kifo cha bwana Singh kinakuja kama aibu kubwa kwa maafisa ambao wanakabiliwa na shinikizo kubwa kuhusu kesi hiyo.
Msemaji wa jela hiyo Sunil Gupta, aliambia BBC kuwa Ram Singh alijinyonga kwa banketi usiku wa kuamkia leo.
No comments:
Post a Comment