ZINEDINE Zidane ni mmoja wa wachezaji wenye kipaji cha aina yake waliowahi kucheza soka akiwa na Ronaldo De Lima.
Akiwa na umri mdogo, Zidane alikuwa na uwezo mkubwa wa kuongoza mashambulizi kupitia katikati ya uwanja huku akitumia uwezo binafsi na nguvu ipasavyo.
Wakati huo alikuwa akichezea klabu ya Bordeux ya Ufaransa kabla hajasajiliwa na Juventus ya Italia kwa ada ya uhamisho ya thamani ya pauni milioni tatu ambazo ni zaidi ya Sh. 7.5 Bilioni.
Akiwa na Juventus, Zidane hakuanza maisha vyema na kulikuwa na watu wengi ambao walikuwa na walakini na uwezo wake.
Kadri msimu wa mwaka 1996/97 ulivyozidi kwenda, Zidane taratibu alianza kuonekana muhimu na alikuwa na mchango mkubwa kwa kikosi kilichofika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ambacho kwa bahati mbaya kilifungwa na Borussia Dortmund ya Ujerumani.
Kipigo hicho kilipokewa kwa mshangao na wengi hasa baada ya Zidane maarufu kama Zizzou kukabwa ‘man to man’ kwenye mchezo huo na kiungo wa Dortmund, Paul Lambert ambaye hii leo ni kocha wa Aston Villa.
.jpg)
Msimu uliofuata, Juventus ilifungwa katika fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid kwa bao la Predrag Mijatovic. Kikosi hiki cha Juventus kilichokuwa na Didier Deschamps, Edgar Davids, Alesandro Del Piero na Zizzou kilikuwa kinaonekana kama kitatawala soka la Ulaya kwa muda mrefu ujao.
Kwenye fainali za Kombe la Dunia 1998, Zidane alilazimika kungoja hadi mchezo wa fainali kisha kufunga mabao yake ya kwanza ya michuano hiyo. Mabao hayo ndiyo yaliyoipa Ufaransa ubingwa wa Dunia kwa mara ya kwanza, na hapa hakukuwa na ubishi kuwa, Zidane alikuwa mchezaji bora mbele ya kizazi cha dhahabu cha wachezaji wa Les Bleus.
Miaka
miwili baadaye, Ufaransa ilitwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Ulaya
licha ya Zidane kutofunga bao hata moja. Hakuna ubishi kuhusu mchango
alioutoa katika mafanikio hayo ya Ufaransa mwaka 2000. MCHEZAJI GHALI KULIKO WOTE DUNIANI

Mwaka 2001 Zidane aliuzwa kwenda klabu ya Real Madrid kwa dau lililoweka rekodi ya Dunia kwa wakati huo la pauni milioni 42 ambazo ni zaidi ya Sh. 105 Bilioni.
Msimu wake wa kwanza akiwa na Real Madrid, ulikuwa mgumu na kulikuwa na taarifa kuwa, presha ya matarajio makubwa yaliyokuwepo mabegani mwake kutokana na fedha nyingi zilizotumika kumsajili ilikuwa kubwa kwake.
Hata hivyo, Real Madrid ilifika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2002 na kwenye fainali yake ya tatu, Zidane alifanikiwa kutimiza ndoto zake.

No comments:
Post a Comment