
Wanwake wengi wamelalamika sana wakisema wanabakwa na watu waliovalia magwanda ya jeshi
Shirika la kutetea haki za
kibinadamu, Human Rights Watch, limesema kuwa makundi yaliyojihami
nchini Somalia ikiwemo majeshi ya serikali, yamefanya vitendo vya
ubakaji, kuwachapa na kuwadhulumu watu walioachwa bila makao au
wakimbizi.
Ripoti ya shirika hilo imegusia wale watu
waliokimbia vita tangu mwaka 2011 kwa sababu ya njaa, na sasa wanaishi
katika kambi mjini Mogadishu.Shirika hilo linasema , kuwa wakimbizi wa ndani, hasa wanawake wameripoti kubakwa na kudhulumiwa na watu waliovalia sare za kijeshi na wengine wanaoaminiwa kuwa wapiganaji wa makundi ya waasi.
Linasema kuwa baadhi ya vitendo vibaya vya dhuluma walivyofanyiwa ni pamoja na dhulma za kingono dhidi ya wanawake na wasichana.
Kadhalika ripoti hiyo imewanukuu wanawake wanaodai kubakwa akiwemo mwanamke mwenye umri wa miaka
23 aitwaye, Quman.
No comments:
Post a Comment