Friday, June 6, 2014

FIFA yatangaza imani na mchuano Brazil


Sepp Blatter wa Fifa
Rais wa shirikisho la soka duniani Fifa amesema kuwa ana imani kuwa kombe la dunia nchini Brazil litakuwa na ufanisi mkubwa.
Bwana Sepp Blatter ametoa wito kwa raia wa Brasil wajitolee vilivyo kusaidia kufanikisha mchezo huo mwaka huu.
Matamshi ya Bwana Blatter yamekuja huku hofu ikielezewa mjini Sao Paulo juu ya msongamano mkubwa wa watu na magari kufuatia mgomo wa wafanyikazi wa shirika la reli.
Maafisa wakuu wa Fifa wenyewe walikwama katika foleni ndefu ya magari barabarani.
Usafiri huo unatarjaiwa kutatizika zaidi kufatia kuvunjika kwa mazungumzo kati ya muungano wa wafanyikazi hao na serikali.
Orodha kamilifu ya timu zitakazoshiriki michuano wa Kombe la Dunia imetolewa. Majina ya makocha 32 ambao watasimamia mechi za mashindano hayo, pia majina ya wachezaji 736 watakaoshiriki mechi hizo zitakazochezwa kati ya Juni 12 hadi Julai 13 zimetangazwa..
Taarifa zaidi iliyotolewa ni kuwa timu zimepunguza idadi ya wachezaji, majeraha kukaguliwa na hali ya afya ya wachezaji kutathminiwa. Haya yote yakiwa ni matayarisho kwa michuano hayo yatakayo anza jijini Sao Paulo.
Timu zote zimetayarisha wachezaji 23 ambao kwa sasa watazingatia uwezo wa kufanikisha timu zao.

3 shot at Seattle Pacific University before student tackles gunman


Victim confirmed dead in Seattle shooting

STORY HIGHLIGHTS- When Briana Clarke heard popping sounds on a Seattle college campus on Thursday, she thought the source must be something innocent -- bursting balloons. Then she saw a classmate running frantically, saying someone had been shot.
A gunman had opened fire at Seattle Pacific University, killing one person and wounding two more before he was tackled by a student security guard, Seattle police said.
The gunman was reloading a shotgun when the tackler, working as a building monitor, used pepper spray and knocked him down, Police Capt. Chris Fowler told reporters.
"Once on the ground, other students jumped on top of them and subdued the shooter," he said.
The suspect, 26-year-old Aaron Ybarra, is not a student at the school, police said.
They believe he acted alone, but the investigation is going on. Police did not disclose a motive.
Clarke saw students covered in blood.
"When I walked outside and saw someone down, that was disturbing seeing a bunch of bullets around," she said. "Seeing my friend outside being treated, that's was hard to swallow."
The thought that she could have been a victim went through her head.
Police are convinced the shooter would have harmed more people, had those around him not intervened.
"This story is not about an evil act but about the people that actually lived through this scenario and assisted each other when things were pretty tragic." said Seattle police Asst. Chief Paul McDonagh.
The suspect was armed with a shotgun, a knife and additional rounds of ammunition, he said.
Pellet wounds
condition
attle college shooting
The shooting began inside the foyer of Otto Miller Hall, which houses the university's science, math and engineering departments, when the gunman confronted three people and shot them, Fowler said.
A 19-year-old man was declared dead at Harborview Medical Center. A 20-year-old woman was in critical condition and a 24-year-old man was in satisfactory , she He suffered pellet wounds to the neck and chest, a police statement said. A fourth person was transported to the hospital with minor injuries.
Officials immediately locked down the campus.
Blood on floor and walls
University President Daniel J. Martin told CNN affiliate KCPQ he turned on a monitor to view security camera images from Otto Miller Hall after he was alerted to the shooting.
"The students acted without regard for their own safety," he said, his voice breaking with emotion.
Jillian Smith was taking a math test when she learned the campus was on lockdown. She said she kept taking the test until she heard police officers yelling.
"After we found out by social media what was going on, people were crying and everything," Smith told CNN affiliate KOMO.
Police escorted students out of the building, where she she saw blood on the floor and walls in the foyer.
Blake Oliveria was in a class when he heard the gunshots.
He said he removed his shoes in case he had to run but stayed in the classroom until police arrived to escort students out.
"I saw blood ... on the ground," he told CNN. "There were two or three big (pools) and some small ones scattered throughout the hallway."
Mary Jones' daughter attends Seattle Pacific but was unharmed. Still, she wonders how safe colleges will be without laws regulating access to guns.
"Where are the controls to keep our children from purchasing a handgun or any other kind of weapon? And does that take government controls to keep that from happening? I don't know," she told KOMO. "There has to be a greater understanding of what that weapon can do and the pain it can inflict on another person's life."
Seattle Pacific is a Christian university with a student population of 4,270. It is located in Seattle's Queen Anne neighborhood. The school has canceled classes all day Friday, it said on its website.
BY foibe omary

Thursday, June 5, 2014

208 wafariki kutokana na Ebola Guin


Maafisa wa afya wakiwazika waathiriwa wa homa ya Ebola
Angaa watu 21 waliaga dunia na visa vingine 37 vinavyohusiana na Ebola kuripotiwa kati ya tarehe 29 mwezi Mei na tarehe 1 mwezi Juni na kufikisha idadi ya visa hivyo kufikia 328 katika taifa hilo lililoko magharibi mwa Afrika.

Hadi sasa, hakuna dawa za kuzuia wala kutibu Ebola- moja kati ya virusi hatari sana duniani.Kati ya visa hivi, 193 vilithibitishwa kupitia vipimo vya maabara.
Zaidi ya nusu ya vifo vya hivi karibuni vilitokea kusini mwa eneo la Guekedou, mahali ambapo ugonjwa huo ulianzia.
Visa vitatu vimedhibitishwa na vingine 10 vinavyodhaniwa kuwa wa ugonjwa huo vimeripotiwa katika nchi Jirani ya Sierra Leone.
Mgonjwa wa Ebola akipokea matibabu
Inaaminika kuwa watu kumi wameaga dunia katika taifa hilo, huku wengine kumi wakifariki nchini Liberia.
Wanaotoa misaada ya matibabu wamesema kuwa sababu moja ya ongezeko la ugonjwa huo ni kuwa watu wanakataa kwenda hospitalini kutibiwa na badala yake kuwaendea waganga.
Homa hiyo ina uwezo ya kuuwa hadi asilimia 90 ya walioathiriwa na huambukizwa wakati maji maji ya mwili, kama vile damu, mkojo na jasho la mtu au mnyama aliyeambukizwa yanapogusana na ya mtu mwingine.
Hata hivyo, binadamu wana nafasi nzuri ya kupona iwapo ugonjwa huo utatambuliwa mapema na kupata matibabu.
Wataalamu kutoka shirika la afya ulimwenguni pamoja na madaktari wasio na mipaka wanaofanya kazi katika eneo hilo wanachunguzwa baada ya uwezekano wa kuathiriwa na Ebola.

DRC yailaumu Rwanda kuwalinda M23


DRC yailaumu Rwanda kuwalinda M2
Afisa mmoja wa Serikali ya DRC ameiambia BBC kuwa imekuwa vigumu kwa serikali yake kuwahoji zaidi ya wapiganaji 500 ambao wamekita kambi nchini Rwanda licha yao kutuma ombi la kufanya hivyo yapata miezi saba iliyopita .
Zaidi ya watu 800,000 walitoroka makwao haswa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo wakati wa mapigano hayo ya wenyewe kwa wenyewe.
Rwanda imekuwa ikipinga madai hayo na kusema kuwa imeshirikiana na serikali ya DRC.
Kundi hilo la M23 lichukua silaha mashariki mwa DRC kuanzia Aprili 2012, liliaumu serikali ya Kinshasa kwa kuwabagua jamii ya watutsi na pia kupuuza makubaliano ya awali ya kusitisha mapigano.
Kundi hilo hata hivyo lilishindwa katika mapigano yaliyoongozwa na jeshi la Umoja wa mataifa likisaidiwa na majeshi ya serikali ya Congo mnamo November 2013.
Wapiganaji hao walitorokea Rwanda na Uganda.
DRC yailaumu Rwanda kuwalinda M23
Katika mji wa Ngoma, mashariki mwa Rwanda mwandishi wetu alikumbana na wapiganaji hao ana kwa ana katika kambi nje ya mji.
Wengi wao wanasema kuwa wamechoshwa na ngoja ngoja hiyo ambayo imedumu kwa kipindi kirefu sasa na wanasema kuwa wangependa kuomba hifadhi nchini Rwanda, kwani wanahofia kurejea ndani ya Congo.
Serikali ya Congo imetangaza kuwa itawapa msamaha wapiganaji hao.
Tulipoingia ndani ya kambi hiyo ,hali na taswira ilikuwa tulivu na shwari .
Kulikuwa na hema kubwa nyeupe, majengo kadha mbali na bustani iliyolindwa na nadhifu.
Wapiganaji hao wanalala sita katika chumba kimoja .
Wanajipikia wenyewe hadharani na hawaruhusiwi kuondoka kambini ila wanapokwenda kupata matibabu.
Japo taswira hiyo ni ya utulivu wapiganaji zaidi ya 100 wametoroka tangu kuzinduliwa miezi 15 iliyopita .
Wapiganaji wa M23 waomba hifadhi Rwanda
Kiongozi wao Jean Marie Runiga hana mipango yeyote ya kutaka kurejea nyumbani.
Runiga ambaye anatuhumiwa kwa mauji ya jinai na DRC ameomba hifadhi nchini Rwanda .
Mwenyewe haishi kambini,anakaa katika jumba alilokodishiwa na serikali karibu na kambi hiyo.
Afisa wa Serikali ya DR Congo Francois Muamba,amesema kuwa Rwanda kinyume na Uganda ,imekuwa ikijivuta sana katika swala kuu la kuwataka wale wanaotuhumiwa kwa mauaji ya halaiki na makosa mengine dhidi ya binadamu kufikishwa mahakamani .
Muamba ameilaumu serikali ya Kigali kwa kuwalinda makamanda wanne wa M23 wanaoshtumiwa kwa kuongoza mauaji ya halaiki nchini DR Congo.
Anasema Rwanda imezuia mahojiano ya wapiganaji hao licha ya kutakiwa kuwawakilisha kwa vyombo vya usalama vya DRC.

Pembe za ndovu zanaswa Mombas


Pembe 228 za ndovu zanaswa Mombasa
Shehena hiyo ya pembe za ndovu 114 ilipatikana katika bohari moja inayotumika na kampuni ya uchukuzi.
Mshukiwa mmoja alikamatwa katika tukio hilo.
Kupatikana kwa shehena hiyo kubwa ya meno ya ndovu inatilia pondo dhana inayotokana na utafiti wa mashirika yanayopigania kusitishwa uuzaji wa pembe za ndovu kuwa bandari za Mombasa Kenya Togo na Dar Salaam
Tanzania zinatumika kusafirisha pembe za ndovu kutoka kote barani Afrika kuelekea bara Asia.
Utashi wa pembe za ndovu na bidhaa zitokanazo na pembe nchini China na mataifa ya Mashariki ya mbali ndio unaochochea mauaji ya tembo katika mbuga na hifadhi mbalimbali barani Afrika.
Maafisa wadai pembe hizo zilikuwa njiani kuelekea Asia
Mbali na kuwa bidhaa ya thamani kubwa huko Asia na China pembe za ndovu hutumika kama dawa ya kienyeji .
Shehena hii ni kubwa zaidi kuwahi kukamatwa mwaka huu bandarini kulingana na afisa wa Huduma kwa wanyama pori nchi Kenya yaani (KWS) Paul Muya.
Afisa wa KWS alidokeza kuwa kuwa shehena hiyo kubwa ya ndovu ilitoka katika moja ya mataifa mbalimbali yanayotumia bandari ya Mombasa kusafirisha bidhaa zao kuelekea ughaibuni.
Mwezi Aprili,Serikali ya Kenya iliwasimamisha kazi kwa muda maafisa wakuu wa shirika la huduma kwa wanyama pori KWS kwa kile ilichotaja kuwa ni utepetevu kazini.
Serikali Kenya wakati huo ilisema kuwa itachukua mstari wa mbele kulinda wanyama pori.
Kulingana na takwimu nchini Kenya vifaru 18 na ndovu 50 wameuawa mwaka huu idadi sawa na ile iliyosajiliwa mwaka uliopita.
Wanaharaki wa kulinda wanyama pori wanadai kuwa idadi hiyo ni chini mno kwani visa vingi haviripotiwi.

Ni uhalifu kuwanyanyasa wanawake - Misri


wanawake wa Misri
Kwa mara ya kwanza Misri imepitisha sheria inayotaja unyanyasaji wa wanawake kuwa uhalifu.
Chini ya sheria hiyo wanaume watafungwa miaka 5 gerezani kwa kuwanyanyasa wanawake hadharani au faraghani.
Sheria hiyo imepitishwa kama hatua ya mwisho kuchukuliwa na rais anayeondoka wa Misri Adly Mansour.
Watetesi wa haki za wanawake nchini Misri wamesema kuwa unyanyasaji wa wanawake umefikia viwango vya kuhuzunisha. Utafiti uliofanywa umeonesha kuwa karibu wanawake wote wa Misri wamewahi kupitia unyanyasaji wa aina fulani iwe ya matusi au hata ubakaji.
Utafiti huo umeonesha kuwa hata mavazi ya kufunika mwili wote yanayopendekezwa na sheria za kiislamu nchini humo, hazijawazuia wanaume hao kuwanyanyasa wanawake.
Na sasa inahofiwa kuwa mapinduzi waliofanya mwaka wa 2011 hayakuleta mabadiliko yoyote.
Wanawake wengi wamelalamika kuwa walinyanyaswa wakiwa katika maandamano katika midani ya Tahrir.
Watetesi hao wa haki wanasema kuwa polisi mara nyingi wanawalaumu waathiriwa kuliko wale wanaofanya uhalifu huo.
Sasa sheria hii inachukuliwa kama hatua kubwa sana kusaidia tatizo hilo, ila hofu ni kwa utekelezaji wake. Wadadisi wanasema kuwa itakuwa vigumu zaidi kubadilisha itikadi za watu juu ya unyanuasaji wa wanawake nchini humo .

Monday, May 5, 2014

Kiongozi wa maandamano Nigeria mbaroni



 
Shule hii ndio waliokuwepo wasichana hao waliotekwa
Mwanaharakati mwanamke aliyekuwa akiongoza maandamano nchini Nigeria kushinikiza serikali ya nchi hiyo kuwaokoa wasichana 200 waliotekwa hivi karibuni ametiwa mbaroni na polisi kwa amri ya mke wa Rais wa nchi hiyo.
Naomi Mutah Nyadar alikuwa miongoni wanawake waliohudhuria mkutano ulioitishwa na ma mke wa rais Patience Jonathan na baadae mwanaharakati huyo alipelekwa kituo cha polisi habari zinasema.